Tuesday, 12 July 2016

IFAHAMU WILAYA YA ROMBO

best coffee beans
Mti wa buni





Mgomba

https://upload.wikimedia.org/wikipedia/en/2/2b/Map_of_Kilimanjaro_Region_%28Rombo_District_highlighted%29.gif
Ramani ya Mkoa wa Kilimanjaro
Rombo ni moja kati ya wilaya 7 zinazounda mkoa wa Kilimanjaro. Imegawanyika katika tarafa 5 zenye jumla ya kata 24. Tarafa hizo ni Tarakea, Usseri, Mashati, Mkuu pamoja na Mengwe. Hapa chini ni majina ya Kata zote za Rombo (W)
  • Aleni
  • Holili
  • Katangara Mrere
  • Kelamfua Mokala
  • Keni Mengeni
  • Kirongo Samanga
  • Kirwa Keni
  • Kisale Msaranga
  • Kitirima Kingachi
  • Mahida
  • Makiidi
  • Mamsera
  • Manda
  • Marangu Kitowo
  • Mengwe
  • Motamburu Kitendeni
  • Mrao Keryo
  • Nanjara Reha
  • Ngoyoni
  • Olele
  • Shimbi
  • Tarakea Motamburu
  • Ubetu Kahe
  • Ushiri Ikuini
Wilaya nyingine za mkoa wa Kilimanjaro ni
Mipaka
·         Upande wa Kaskazini na Mashariki Rombo imepakana na Nchi ya Kenya
·         Upande wa Magharibi wilaya ya Rombo imepakana na wilaya za Siha na Hai
·         Upande wa Kusini wilaya ya Rombo imepakana na wilaya ya Moshi vijijini
Idadi ya watu: Rombo inakadiriwa kuwa na idadi ya watu takribani 260,963 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012.
Mazao makuu: Rombo ni kati ya wilaya maarufu nchini Tanzania kwa kilimo cha zao la Ndizi na Buni aina ya arabika.
Utamaduni: Rombo kama ilivyo kwa wilaya nyingine za Mkuoa wa Kilimanjaro, ni kati ya wilaya ambazo mwamko wa kielimu upo juu tangu zamani. Hata hivyo siku za karibuni ulevi wa pombe za kienyeji umeshamiri sana hali ambayo inchangia kupungua kwa uzalishaji katika kilimo na hata wakati mwingine baadhi ya watoto kulazimika kukatisha masomo kutokana na hali duni ya kimaisha. Baadhi ya majina ya pombe hizo ni pamoja na Mbege, Dadii, Busa, Kimorali, Kamchape, Ngongo, Banana, Chibuku pamoja na pombe zilizorasimishwa.
Vyakula vya kiasili katika wilaya ya Rombo ni vile vinavyotokana na ndizi kwa mfano Machalari, Kiburu, Kena, Mtori, Ng’ande, Irembwe hutengenezwa kwa kutumia mbaazi,maharagwe au kunde, pamoja na Ngararimo ambazo hutengenezwa kwa kutumia mahindi…….
Nini Kisichofahamika kuhusu Rombo ???????????
Kama nilivyoeleza hapo juu, hali ya Unywaji wa pombe kwa rika zote umekuwa ukiongeaeka katika karne hii ya 21 hususani kwa kati ya miaka 10 iliyopita kwa sababu mbalimbali zikiwepo msongo wa mawazo, udadisi pamoja msukumo wa marafiki (Peer presure)

1. JE, UNADHANI NINI KIFANYIKE ILI KUKINUSURU KIZAZI CHA SASA DHIDI YA MATUMIZI MAKUBWA YA POMBE ?????????

2. JE, TATIZO HILI LAWEZA KUISHA???????

3. JE, NANI ALAUMIWE KUTOKANA NA TATIZO HILI??????

4. JE, NINI MAONI YAKO DHIDI YA MATUMIZI YA POMBE??????

5. JE, POMBE INA MADHARA GANI KATIKA UKUAJI WA UCHUMI WA TAIFA NA JAMII ILIYOSTAARABIKA???????










No comments:

Post a Comment