![]() Mti wa buni |
---|
![]() | ||||
---|---|---|---|---|
![]() Ramani ya Mkoa wa Kilimanjaro Rombo ni moja kati ya wilaya 7 zinazounda mkoa wa Kilimanjaro. Imegawanyika katika tarafa 5 zenye jumla ya kata 24. Tarafa hizo ni Tarakea, Usseri, Mashati, Mkuu pamoja na Mengwe. Hapa chini ni majina ya Kata zote za Rombo (W)
Wilaya nyingine za mkoa wa
Kilimanjaro ni
Mipaka
·
Upande wa Kaskazini na Mashariki Rombo
imepakana na Nchi ya Kenya
·
Upande wa Magharibi wilaya ya Rombo
imepakana na wilaya za Siha na Hai
·
Upande wa Kusini wilaya ya Rombo
imepakana na wilaya ya Moshi vijijini
Idadi
ya watu: Rombo inakadiriwa kuwa na idadi ya watu takribani 260,963 kwa mujibu
wa sensa ya mwaka 2012.
Mazao
makuu: Rombo ni kati ya wilaya maarufu nchini Tanzania kwa kilimo cha zao la
Ndizi na Buni aina ya arabika.
Utamaduni:
Rombo kama ilivyo kwa wilaya nyingine za Mkuoa wa Kilimanjaro, ni kati ya
wilaya ambazo mwamko wa kielimu upo juu tangu zamani. Hata hivyo siku za
karibuni ulevi wa pombe za kienyeji umeshamiri sana hali ambayo inchangia
kupungua kwa uzalishaji katika kilimo na hata wakati mwingine baadhi ya watoto
kulazimika kukatisha masomo kutokana na hali duni ya kimaisha. Baadhi ya majina
ya pombe hizo ni pamoja na Mbege, Dadii, Busa, Kimorali, Kamchape, Ngongo,
Banana, Chibuku pamoja na pombe zilizorasimishwa.
Vyakula
vya kiasili katika wilaya ya Rombo ni vile vinavyotokana na ndizi kwa mfano
Machalari, Kiburu, Kena, Mtori, Ng’ande, Irembwe hutengenezwa kwa kutumia
mbaazi,maharagwe au kunde, pamoja na Ngararimo ambazo hutengenezwa kwa kutumia
mahindi…….
Nini Kisichofahamika
kuhusu Rombo ???????????
Kama
nilivyoeleza hapo juu, hali ya Unywaji wa pombe kwa rika zote umekuwa
ukiongeaeka katika karne hii ya 21 hususani kwa kati ya miaka 10 iliyopita kwa
sababu mbalimbali zikiwepo msongo wa mawazo, udadisi pamoja msukumo wa marafiki
(Peer presure)
1. JE, UNADHANI NINI KIFANYIKE ILI KUKINUSURU KIZAZI CHA
SASA DHIDI YA MATUMIZI MAKUBWA YA POMBE ?????????
2. JE, TATIZO HILI LAWEZA KUISHA???????
3. JE, NANI ALAUMIWE KUTOKANA NA TATIZO HILI??????
4. JE, NINI MAONI YAKO DHIDI YA MATUMIZI YA POMBE??????
5. JE, POMBE INA MADHARA GANI KATIKA UKUAJI WA UCHUMI WA
TAIFA NA JAMII ILIYOSTAARABIKA???????
| ||||
No comments:
Post a Comment