Saturday, 16 July 2016

TCU YATOA MAELEZO YA MAREKEBISHO KUHUSU SIFA ZA KUDAHILIWA KUSOMA SHAHADA MWAKA HUU

















 

Tume ya vyuo vikuu nchini Tanzania imejitokeza leo tarehe 16  July 2016 na kutolea maelezo kuhusu utata ulikuwepo kuhusu wakina nani wana sifa ya kusoma degree kwa mwaka wa masomo 2016/17.....
Kwa mujibu wa tangazo lilotolew kwa umma na Katibu mtendaji wa TCU hivi leo ni kuwa tofauti na ilivyoeleweka mara baada ya marekebisho ya vigezo vya kusoma shahada hapa nchini, kwamba ni lazima kupata D mbili ili udahiliwe sio sahihi.....

Kwa mujibu wa tangazo hilo, inatakiwa mhitimu wa kidato cha sita awe najumla ya point 4 katika masomo mawili kati ya matatu ya mchepuo aliosoma......Hivyo mtu aliye na Ufaulu wa C na E atasoma shahada....
Mchanganuo kwa mwaka 2013 kurudi nyuma na mwaka 2016 , A=5, B=4, C=3, D=2, E= 1
Kwa wahitimu wa mwaka 2014-2015, matokeo yao yalukuwa katika mfumo tofauti..Kwao A=A=5, B+=B=4, B=C=3, C=D=2, D=E=1..............Kwa sababu hii, ilivyohesabika awali kuwa ni lazima kuwa na D mbili ndio udahiliwe sio sahihi.....Kwa maelezo zaidi tembelea kiungo cha tovuti ya TCU hapa chini.
 www.tcu.go.tz

Tuesday, 12 July 2016

IFAHAMU WILAYA YA ROMBO

best coffee beans
Mti wa buni





Mgomba

https://upload.wikimedia.org/wikipedia/en/2/2b/Map_of_Kilimanjaro_Region_%28Rombo_District_highlighted%29.gif
Ramani ya Mkoa wa Kilimanjaro
Rombo ni moja kati ya wilaya 7 zinazounda mkoa wa Kilimanjaro. Imegawanyika katika tarafa 5 zenye jumla ya kata 24. Tarafa hizo ni Tarakea, Usseri, Mashati, Mkuu pamoja na Mengwe. Hapa chini ni majina ya Kata zote za Rombo (W)
  • Aleni
  • Holili
  • Katangara Mrere
  • Kelamfua Mokala
  • Keni Mengeni
  • Kirongo Samanga
  • Kirwa Keni
  • Kisale Msaranga
  • Kitirima Kingachi
  • Mahida
  • Makiidi
  • Mamsera
  • Manda
  • Marangu Kitowo
  • Mengwe
  • Motamburu Kitendeni
  • Mrao Keryo
  • Nanjara Reha
  • Ngoyoni
  • Olele
  • Shimbi
  • Tarakea Motamburu
  • Ubetu Kahe
  • Ushiri Ikuini
Wilaya nyingine za mkoa wa Kilimanjaro ni
Mipaka
·         Upande wa Kaskazini na Mashariki Rombo imepakana na Nchi ya Kenya
·         Upande wa Magharibi wilaya ya Rombo imepakana na wilaya za Siha na Hai
·         Upande wa Kusini wilaya ya Rombo imepakana na wilaya ya Moshi vijijini
Idadi ya watu: Rombo inakadiriwa kuwa na idadi ya watu takribani 260,963 kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2012.
Mazao makuu: Rombo ni kati ya wilaya maarufu nchini Tanzania kwa kilimo cha zao la Ndizi na Buni aina ya arabika.
Utamaduni: Rombo kama ilivyo kwa wilaya nyingine za Mkuoa wa Kilimanjaro, ni kati ya wilaya ambazo mwamko wa kielimu upo juu tangu zamani. Hata hivyo siku za karibuni ulevi wa pombe za kienyeji umeshamiri sana hali ambayo inchangia kupungua kwa uzalishaji katika kilimo na hata wakati mwingine baadhi ya watoto kulazimika kukatisha masomo kutokana na hali duni ya kimaisha. Baadhi ya majina ya pombe hizo ni pamoja na Mbege, Dadii, Busa, Kimorali, Kamchape, Ngongo, Banana, Chibuku pamoja na pombe zilizorasimishwa.
Vyakula vya kiasili katika wilaya ya Rombo ni vile vinavyotokana na ndizi kwa mfano Machalari, Kiburu, Kena, Mtori, Ng’ande, Irembwe hutengenezwa kwa kutumia mbaazi,maharagwe au kunde, pamoja na Ngararimo ambazo hutengenezwa kwa kutumia mahindi…….
Nini Kisichofahamika kuhusu Rombo ???????????
Kama nilivyoeleza hapo juu, hali ya Unywaji wa pombe kwa rika zote umekuwa ukiongeaeka katika karne hii ya 21 hususani kwa kati ya miaka 10 iliyopita kwa sababu mbalimbali zikiwepo msongo wa mawazo, udadisi pamoja msukumo wa marafiki (Peer presure)

1. JE, UNADHANI NINI KIFANYIKE ILI KUKINUSURU KIZAZI CHA SASA DHIDI YA MATUMIZI MAKUBWA YA POMBE ?????????

2. JE, TATIZO HILI LAWEZA KUISHA???????

3. JE, NANI ALAUMIWE KUTOKANA NA TATIZO HILI??????

4. JE, NINI MAONI YAKO DHIDI YA MATUMIZI YA POMBE??????

5. JE, POMBE INA MADHARA GANI KATIKA UKUAJI WA UCHUMI WA TAIFA NA JAMII ILIYOSTAARABIKA???????










YANGA WAADHIBIWA DOLA 5000 BADALA YA 10000






Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), limeipiga faini ya dola 5,000 Klabu ya Young African kwa kosa la kuchelewesha mchezo baada ya wachezaji wake kumzonga mwamuzi wakati mchezo wa kuwania kuingia hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho dhidi ya GD Sagrada Esperanca uliofanyika Angola Mei 18, 2016.

Uamuzi wa mchezo huo Na. 100 ulifanywa na Kamati ya Nidhamu ya CAF inayoundwa Mwenyekiti Raymond Hack – Raia wa Afrika Kusini na wajumbe Mustapha Samugabo (Burundi) na Gbenga Elegbeleye (Nigeria). Pia alikuwako Amina Kassem kutoka Sekretarieti ya CAF ambaye ni Mtawala katika Kitengo cha Nidhamu.

Katika mkutano huo uliofanyika Cairo, Misri – Makao Mkuu ya CAF, Julai 3, 2016, kamati ilipitia taarifa zote za mchezo na kufikia uamuzi wa kuipiga faini Young Africans.

Taarifa za mchezo zinasema, wachezaji wa Young Africans walionyesha utovu wa nidhamu kwa kumzonga mwamuzi na kumsukuma mara baada ya kutoa adhabu ya penalti kwa wapinzani. Kwa tukio hilo, mchezo huo ulisimama kwa dakika sita. Polisi waliingia uwanjani kudhibiti hali hiyo.

Kwa kosa hilo, Wachezaji wa Young Africans walivunja Ibara ya 82 inayozungumza utaratibu wa mawasiliano. Kwamba chama chochote cha mpira wa miguu, klabu, ofisa au mtu yoyote wakiwamo wachezaji, lazima waheshimu utaratibu za kuvumilia, uadiliufu na uanamichezo.

Kwa mujibu wa Kamati hiyo ya Nidhamu ya CAF, Young Africans ilistahili kutozwa faini ya dola 10.000 za Marekani kwa makosa ambayo si uungwana kwenye soka yaliyoonyeshwa na wachezaji wake.

Lakini kwa kuwa Young Africans haikuonyesha utovu wa nidhamu katika mchezo mingine ya kimataifa iliyofuata dhidi ya MOB ya Algeria na TP Mazembe ya DRC, imepunguziwa adhabu na sasa wametakiwa kulipa dola 5,000 za Marekani kama faini. Faini hiyo haina budi kulipwa mara moja. Na imetakiwa kuendelea kuwa na nidhamu, vinginevyo adhabu hiyo itawarudia.


Yanga wanayo fursa ya kukata rufaa dhidi ya adhabu hiyo, vinginevyo wanapaswa kuilipa mara moja ili isihesabiwe wamekaidi

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA BAADA YA CR7 NA TIMU YAKE KUREJEA URENO


 3627C74B00000578-3684274-The_Portugal_bus_arrives_at_the_airport_as_the_country_s_heroes_-a-114_1468241690596

Usiku wa 2016 July 10 timu ya taifa ya Ureno ilifanikiwa kushinda Kombe la mataifa ya Ulaya a.k.a Euro, kwa kuinyuka timu ya taifa ya Ufaransa goli 1-0, goli ambalo lilifungwa na na Eder dakika ya 109 katika uwanja wa Stade de France.
3627C23900000578-3684274-Ronaldo_and_Nani_enjoy_the_celebrations-a-119_1468241690836
Baada ya ushindi huo July 11 2016 kikosi cha timu ya taifa ya Ureno kiliwasili Lisbon Ureno wakiwa na Kombe lao na kupata mapokezi makubwa kutoka kwa raia wa nchi hiyo, Ronaldo na wachezaji wenzaji waliwasili Ureno na kutembeza Kombe wakiwa katika basi la wazi.
Tazama picha hapa chini kisha tuambie kipi kifanyike kwa timu ya Taifa TANZANIA yaani TAIFA STARS ili siku moja macho yote Africa yaelekezwe Tanzania


3629C5E100000578-3684274-image-a-143_1468244718738


3628CB1900000578-3684274-Cristiano_Ronaldo_holds_aloft_the_European_Championship_title_af-a-116_1468241690686

Pamoja na kuwa Ufaransa waliweza kusakata kabumbu safi mwisho wa dak 120 ushindi ulilazimika kwenda kwa mshindi kwani ndivyo zilivyo sheria za soka duniani.





UHARIBIFU DARAJA-KIGAMBONI


JE, UMEIKOSA VIDEO FUPI YA UHARIBIFU ULIOTOKEA BAADA YA LORI KUPINDUKA DARAJA LA KIGAMBONI?
 
Ilitokea ajali ya Lori lililokua na Kontena kwenye daraja la Nyerere Kigamboni Dar es salaam usiku wa kuamkia July 11 2016 ambapo ajali hiyo imesababisha majeruhi pamoja na eneo la barabara kuharibiwa, Meneja msimamizi kwenye hili daraja Gerald Sondo alipohojiwa kuhusiana na ajali hiyo alisema tangu daraja hilo maarufu kama Daraja la Nyerere kuanza kutumika hiyo ilikuwa ajali ya kwanza kubwa kuwahi kutokea katika daraja hilo. Ajali hiyo ilisababishwa na gari aina ya SEMI TRAIOLER iliyoacha njia yake na kuzigonga kingo za barabara mojawapo katika flyover (Mandela Road)
Gari hilo lilikuwa likitokea  maeneo ya kigamboni kuelekea mjini. Kutokana na kanuni na taratibu za usimamizi wa daraja hilo, Meneja msimamizi alisema kuwa Uongozi utafanya tathmini ya uharibifu ili matengenezo yaweze kufanyika, lakini pia akasisitiza kuwa baada ya taratibu za kiserikali na kipolisi kukamilika, mhusika aliyesababisha ajali hiyo atawajibika kulipia gharama zote za matengenezo.,,,,,...Tembelea link hapa nchini kwa maelezo zaidi
http://youtu.be/-Wa2GqzcIC4

Monday, 11 July 2016

Ex-St Joseph njaa

WAHANGA WA MKASA WA ST JOSEPH WAMALIZA SEMESTER BILA ''......
Mnamo tarehe 19 Feb 2016 tume ya vyuo vikuu ilifungia vyuo shiriki viwili vya Chuo kikuu cha Mt Joseph kutokana na kushindwa kutekeleza matakwa ya mkataba wa utoaji elimu hapa nchini Tanzania.
Kutokana na hatua hiyo ya serikali kuvifungia vyuo hivyo vishiriki ambavyo ni St Joseph University College of Agricultural science and Technology, Songea na St Joseph University College of Information Tehnology, Songea, ililazimika wanafunzi hao kuhamishiwa katika vyuo vikuu vingine ambavyo ni SUA, RUCU pamoja na UDOM.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida,wakati vyuo vishiriki hivyo vikifungwa serikali kupitia TCU yaani Tanzania Commission of Universities iliahidi kuwa wanafunzi wangelipwa gharama zote za uhamisho jambo ambalo limegeuka kuwa kitendawili kisichojibika....Sambamba na hilo jambo linalotusikitisha sana uongozi wa Maramba media kama wadau wa elimu Tanzania ni kuwa tangu wanafunzi hao wahamishwe hadi wakati tukichapisha habari hii, zaidi ya wanafunzi 300 walio kati ya wanafunzi waliohamishiwa SUA hawajalipwa fedha zao za kujikimu kutoka HESLB ambayo ndiyo taasisi inayosimamia jambo hilo....Baadhi ya wanafunzi tuliohojiana nao wamedai kuwa hakuna majibu yoyote ya kuridhisha kutoka chuoni hapo wala HESLB......Kama wadau wa elimu Tanzania MARAMBA MEDIA tunapenda kutoa rai yetu kwa Waziri wa elimu Prof Joyce Ndalichako aweze kuliangalia jambo hili kwa mapana yake , pamoja na taasisi husika kwani pasipo hivyo Taifa litashindwa kufikia malengo.