Sunday, 6 May 2018

Tanzia

May 6, 2018 ni siku moja kabla ya kuanza kwa mitihani ya kidato cha 6 nchini Tanzania, mwanafunzi mmoja ajiua kwa kujinyonga katika mti wa mwembe.

Mwanafunzi huyo Robert Masaba (21) ni mmoja wa wanafunzi waliohamishwa kutoka shule ya sekondari Nyakato manispaa ya Bukoba kwenda Kahororo baada ya shule ya Nyakato kuharibiwa na tetemeko lililokumba mkoa wa Kagera miaka 2 iliyopita, lililoanza mnamo 10 September 2016.

Aidha,mwanafunzi Robert(marehemu) mwenyeji wa wilaya ya Kwimba mkoa wa Mwanza alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliotegemewa kuanza mitihani yao ya kuhitimu kidato cha sita hapo kesho 2018 May 7.

Bado haijathibitika kwanini ameamua kufanya kitendo hicho kilicho kinyume na haki ya kuishi.
Mungu awasaidie waliobakia wafanye vema mitihani yao.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa; jina la Bwana na libarikiwe.

No comments:

Post a Comment