CAMEROON GIZA NENE
Jan 14 2018 kivumbi cha Afcon kitaanza kutimka kule Gambia. Hata hivyo, wakati mataifa shiriki yakiwa katika maandalizi, Cameroon huenda ikawakosa nyota wake saba kutokana na kile kocha wake Hugo Broos amekieleza kuwa ni maslahi binafsi ya nyota hao.
Nyota hao ni Beki mahiri wa Liverpool Joe Matip, Allan Nyom wa West Bromwich, Andre Onana wa Ajax Amsterdam, Guy N'dy Assembe wa Nancy, Maxime Poundje wa Girondins Bordeaux, Andre-Frank Zambo Anguisa wa Olimpique Marseille pamoja na Ibrahim Amadou wa Lille
(Chanzo: BBC)
REAL MADRID YAPATA AHUENI
Real Madrid imepunguziwa adhabu iliyotolewa na Fifa kutokana na kosa la kukiuka kanuni za usajili wa wachezaji wa umri wa chini ya miaka 18
Mahakama ya usuluhishi wa michezo(CAS) imewapunguzia adhabu hiyo kutoka kutosajili hadi Jan 2018 na badala yake kuanza usajili baada ya July 2017. Pia faini waliyotozwa na Fifa kwa kosa hilo imepunguzwa kutoka pauni 282,000 hadi Pauni 188,000.
VARY KUKOSA MECHI TATU
Mshambuliaji wa Leicester City Jamie Vardy atalazimika kukaa nje ya Dimba hadi Jan 7 2018 ambapo atarejea wakati wa mchezo wao dhidi ya Everton kombe la FA mzunguko wa 3.
Hii ni baada ya rufaa ya timu yake kutupiliwa mbali na FA. Vardy alipewa kadi nyekundu alipomchezea vibaya Mame Diouf.
Michezo atakayoikosa Vardy ni ule wa Everton utakaochezewa ugenini katika dimba la Goodson Park, wa West Ham pale King Power na wa Middles brough Jan 02 018.
VPL MWISHO WA WIKI
Ijumaa hii 23Dec utakuwepo mtanange wa African Lyon vs Yanga watakaomenyana pale Shamba la Bibi saa kumi na nusu jioni.
Jumamosi 24Dec;
Majimaji vs Azam Fc uwanja wa Majimaji saa kumi kamili jioni.
Mwadui Fc vs Mbao Fc uwanja wa Mwadui Complex saa kumi kamili jioni.
Simba Sc vs JKT Ruvu Shamba la Bibi saa kumi kamili jioni.
©marambamedia.blogspot.com2016
No comments:
Post a Comment