Friday, 23 December 2016

Heri ya Krismasi na Mwakampya 2017

Anaandika *Nascent Franzwa*
Jmos Dec 24 2016

*Christmass ikufanye mtu bora*

Tarehe 25 kila Dec ni siku ambayo Wa Kristo walio wengi huitumia siku hiyo wakikumbuka ujio wa Masiha kwa mara ya kwanza duniani kupitia kwa Bikira aitwaye Marimu, zaidi ya miaka 2000 iliyopita.

Watu wengi huitumia siku hii kwa namna mbali mbali ikiwepo kufurahia na familia zao, kutembelea maeneo mbali mbali na kwa kusali.

Mara kadhaa katika sikukuu kubwa kama hii vimekuwepo visa kadhaa ambavyo vimekuwa vikisababisha maafa mathalani kuwaachia watoto kwenda katika kumbi za starehe za watoto ambazo hazina ubora na ulinzi wa kutosha.

Kama wazazi tunajukumu la kuhakikisha kuwa tutaacha vitabia hivyo na kuwa watu wapya kwa kuwa karibu zaidi na watoto wetu hasa wadogo ili kuepusha changamoto za maafa kwa watoto kujirudia.

Uongozi wa Marambamedia unawatakia watu wote sherehe njema za Kuzaliwa Kristo pamoja na Mwakampya wenye heri na fanaka.

Tuoneshe upendo kwa wote

©Marambamedia2016

No comments:

Post a Comment