Friday, 23 December 2016

Heri ya Krismasi na Mwakampya 2017

Anaandika *Nascent Franzwa*
Jmos Dec 24 2016

*Christmass ikufanye mtu bora*

Tarehe 25 kila Dec ni siku ambayo Wa Kristo walio wengi huitumia siku hiyo wakikumbuka ujio wa Masiha kwa mara ya kwanza duniani kupitia kwa Bikira aitwaye Marimu, zaidi ya miaka 2000 iliyopita.

Watu wengi huitumia siku hii kwa namna mbali mbali ikiwepo kufurahia na familia zao, kutembelea maeneo mbali mbali na kwa kusali.

Mara kadhaa katika sikukuu kubwa kama hii vimekuwepo visa kadhaa ambavyo vimekuwa vikisababisha maafa mathalani kuwaachia watoto kwenda katika kumbi za starehe za watoto ambazo hazina ubora na ulinzi wa kutosha.

Kama wazazi tunajukumu la kuhakikisha kuwa tutaacha vitabia hivyo na kuwa watu wapya kwa kuwa karibu zaidi na watoto wetu hasa wadogo ili kuepusha changamoto za maafa kwa watoto kujirudia.

Uongozi wa Marambamedia unawatakia watu wote sherehe njema za Kuzaliwa Kristo pamoja na Mwakampya wenye heri na fanaka.

Tuoneshe upendo kwa wote

©Marambamedia2016

Tuesday, 20 December 2016

MichezoniLeo2016Dec21

CAMEROON GIZA NENE
Jan 14 2018 kivumbi cha Afcon kitaanza kutimka kule Gambia. Hata hivyo, wakati mataifa shiriki yakiwa katika maandalizi, Cameroon huenda ikawakosa nyota wake saba kutokana na kile kocha wake Hugo Broos amekieleza kuwa ni maslahi binafsi ya nyota hao.

Nyota hao ni Beki mahiri wa Liverpool Joe Matip, Allan Nyom wa West Bromwich, Andre Onana wa Ajax Amsterdam, Guy N'dy Assembe wa Nancy, Maxime Poundje wa Girondins Bordeaux, Andre-Frank Zambo Anguisa wa Olimpique Marseille pamoja na Ibrahim Amadou wa Lille
(Chanzo: BBC)

REAL MADRID YAPATA AHUENI
Real Madrid imepunguziwa adhabu iliyotolewa na Fifa kutokana na kosa la kukiuka kanuni za usajili wa wachezaji wa umri wa chini ya miaka 18

Mahakama ya usuluhishi wa michezo(CAS) imewapunguzia adhabu hiyo kutoka kutosajili hadi Jan 2018 na badala yake kuanza usajili baada ya July 2017. Pia faini waliyotozwa na Fifa kwa kosa hilo imepunguzwa kutoka pauni 282,000 hadi Pauni 188,000.

VARY KUKOSA MECHI TATU
Mshambuliaji wa Leicester City Jamie Vardy atalazimika kukaa nje ya Dimba hadi Jan 7 2018 ambapo atarejea wakati wa mchezo wao dhidi ya Everton kombe la FA mzunguko wa 3.
Hii ni baada ya rufaa ya timu yake kutupiliwa mbali na FA. Vardy alipewa kadi nyekundu alipomchezea vibaya Mame Diouf.
Michezo atakayoikosa Vardy ni ule wa Everton utakaochezewa ugenini katika dimba la Goodson Park, wa West Ham pale King Power na wa Middles brough Jan 02 018.

VPL MWISHO WA WIKI
Ijumaa hii 23Dec utakuwepo mtanange wa African Lyon vs Yanga watakaomenyana pale Shamba la Bibi saa kumi na nusu jioni.

Jumamosi 24Dec;
Majimaji vs Azam Fc uwanja wa Majimaji saa kumi kamili jioni.

Mwadui Fc vs Mbao Fc uwanja wa Mwadui Complex saa kumi kamili jioni.

Simba Sc vs JKT Ruvu Shamba la Bibi saa kumi kamili jioni.

©marambamedia.blogspot.com2016

Habari Kuu 20 Dec

Trump aidhinishwa rasmi kuwa Rais wa 45 wa Marekani.

Siku 32 za kupotea kwa Mwanaharakati wa Chama Kikuu cha upinzani nchini Tanzania , CHADEMA ,Ndg Ben Saanane bado ni fumbo zito.

Balozi wa Urusi nchini Uturuki Bwana Andrey Karlov auawa kwa kupigwa risasi akiwa katika ufunguzi wa maonesho ya sanaa. Rais Vladimir Putin amekitaja kitendo hicho kama uchokozi.

Mkurugenzi mtendaji wa mtandao maarufu Afrika Mashariki na Kati Jamii Forum Ndugu Maxence Melo aachiwa huru kwa dhamana huko nchini Tanzania.

Nchini DRC milio ya risasi imesikika maeneo kadhaa ya miji ikiwemo miji nikiwa ya Kinshasa na Lubumbashi kutokana na kutokuelewana kati ya upinzani na serikali juu ya muda wa nyongeza wa Joseph Kabila kusalia madarakani baada ya muhula wake kuisha usiku wa kuamkia Leo 20 Dec 2016.

Ripoti za shirika la Afya duniani zimeeleza kuwa, idadi inayokadiriwa kuwa sawa na nusu ya watu wazima barani Afrika wanakabiliwa na tatizo la Shinikizo la damu (Pressure) na hivyo kuifanya Afrika kuwa na kiwango cha juu cha tatizo hilo duniani kwa mujibu wa WHO.

Katika Michezo: Mwanadada Evelyene Njambi Thungu kutoka Kenya ameingia katika orodha ya warembo watano bora katika shindano la Malkia wa urembo duniani 2016 lililofanyika huko Marekani. Kwa sasa ndiye Malkia wa urembo barani Afrika.

SAKATA LA BEN SAANANE

Ikiwa zimepita siku 32 tangu kupotea katika katika namna isiyoeleweka kwa Mwanaharakati Ben Rabiu Wa Saanane mnamo Nov 18, 2016, hizi ni baadhi ya dhahania zilizopo katika mawazo ya Watanzania wengi.

Suala hili naligawanya katika matabaka 3 (yenye kujengwa na dhahania siyo uhalisia)., na matabaka hayo yote yana nguvu kubwa ya hisia hasi au chanya kuhusu sakata hili la ndugu yetu huyu.., nitafafanua matabaka ya fikra na hisia zangu kama Ifuatavyo ;

(I) BEN RABIU WA SAANANE AMETEKWA?; Hii ni moja kati ya hofu yangu kuu sana, hofu hii inachagizwa na namna ya mkingamo wa hali ya kisiasa katiia bara la Afrika kwa wanasiasa wa upinzani, wanaharakati na wakosoaji wakubwa wa tawala za kiafrika, hutendwa vibaya sana na matabaka dola.., wanasiasa hawa ambao huonesha dhahiri rangi zao (kwa aina ya siasa ambayo huchagua kuitumia,) hukumbwa na madhara sana., ipo mifano mingi sana ya watu katika mataifa ya Afrika ambao walipotea, baadae ikaja kujulikana maiti zao zimetelekezwa au wao kupatikana wakiwa hai...,

Bara la Afrika ndilo lenye kuongoza kwa kupotea kwa wanaharakati, wanasiasa, waandishi wa habari na wakosoaji wenye mrengo na msimamo mkali dhidi ya vyama dola au serikali.., makundi hayo ndiyo yenye kuathirika sana.., watawala wengi hawapendi kuona ukosoaji dhidi yao, wafuasi wa watawala hao mara nyingi sana hutumia mamlaka zao kuwapa shuruba wakosoaji hao.., kuwateka, kuwatesa na Mara nyingine kuwaua kabisa (mifano mingi sana inapatikana katika nchi za bara hili la Afrika).., hofu ya kupotea kwa njia kuwekwa kwa ndugu yetu huyu ni kubwa sana!

katika dhahania hii kuna maswali kadhaa ya kujiuliza;

(a) nani amemteka Ben Rabiu Wa Saanane..,?
(b) kwanini Ben atekwe na watu hao wasiojulikana..,?
(c) kwani Ben ana hatarisha usalama wa nani hadi atekwe na watu wasiojulikana!?
(d) kama ametekwa kweli..  Kwanini watesi wake wasimuachie huru sasa au watelekeze maiti yake!?

.., majibu ya maswali hayo siwezi kuwa nayo hata kidogo.., lakini bado akili yangu na akili ya watu wengine inaweza kuendelea kuhoji na hata kuamini BEN ametekwa!

(II) BEN RABIU WA SAANANE, ANATEKELEZA SHUGHULI ZA CHAMA CHAKE; kuna akili nyingine katika dhahania zangu inaeleza wazi.., huyu mtu wetu atakuwa yuko salama salmini anatekeleza shughuli zake za chama.., kwa sababu gani...., chama chake (CHADEMA) kimewahi/hadi sasa ni mwajiri wa Ben Rabiu wa Saanane.., Ben amewahi kuhudumu pale Ufipa (makao makuu ya CDM) kama mkurugenzi wa idara ya utafiti, sera na mambo ya nje (kama sijakosea).., ingawa kuna taarifa zinakuja (zisizo rasmi sana) kwamba kitengo hicho kilifutwa katika teuzi mpya za wakurugenzi wa idara katika chama hicho.., hivyo BEN akabaki kuwa msaidizi binafsi (personal Secretary) wa mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Aikaeli Mbowe.., hadi hapo., luna maswali kadhaa naweza sasa kujiuliza mwenyewe hapa;

(a) kwanini Mbowe ambaye huyu (BEN) ni mtumishi wake binafsi (msaidizi binafsi), yupo kimya kuhusu suala hili hadi sasa..,!?
(b) kwanini CHADEMA, chama cha Ben (kama mwanachama) na mtumishi wa zamani wa chama hicho, hakioneshi 'aggressiveness' ya kutosha katika suala hili!?
(c) kwanini Chama na wanachama (baadhi) hawaoneshi kubeba suala hili kama ajenda yao mtambuka (hata kwa kufungua kesi ya kufukua miili ile 7 ileliyozikwa kule Bagamoyo) kutambua kama kuna BEN katika wale!?
(d) wabunge na wanachama wakubwa wale waamdamizi, hawaoneshi kabisa morali chanya ya kuandika katika mitandao, katika vyombo vya habari kuhusu kupotea kwa BEN.., kwa nini!?

Maswali hayo 4, mimi sina majibu nayo hata kidogo, na ndiyo maana namaliza kwa kuuliza.., na ndiyo maana nafika kwenye hitimisho la dhahania hiyo kwa kusema "labda..., BEN yupo salama, na viongozi wake, rafiki zake (baadhi) na hata ndugu zake wanatambua huyu mtu alipo"..,

Katika dhahania hii kuna ukiznzani.., ndugu wa BEN ndiyo walikuwa watu wa kwanza kabisa kuanza kupata hofu ya mahali alipo ndugu yao (wakatoa taarifa kwa marafiki wa BEN, na baadae polisi) hivyi inawezekana hawa hawatambui ndugu yao alipo.., swali la kujiuliza.., BEN yuko katika shughuli zake binfasi (labda) za masomo bila kujulisha ndugu zake!? Je, BEN yuko katika shughuli za chama bila kuwapa taarifa ndugu, jamaa na marafiki zake wa karibu!? KWELI INAWEZEKANA!?

(III) BEN RABIU WA SAANANE, AMEAMUA KUJIWEKA MBALI NA MKONDO WA KISIASA; dhahania yangu ya mwisho kabisa ni kwamba; huyu msomi, mwanasiasa na kijana machachari mwenye weledi wa kutosha, ameamua kujiweka mbali na siasa.., kama ambavyo tunajua na kutambua..,

siasa za Afrika ni siasa zenye mapungufu mengi.., majungu, fitina, kebehi na kukatishana tamaa sana.., ni siasa zenye kupoteza muda wa wale ambao ni 'underdog' katika siasa.., ni aina ya siasa ambazo 'wale waliofanikiwa kisiasa hawapendi kuona wanasiasa wapya nyuma yao'...., pia ni aina ya siasa ambayo hutengeneza wafuasi na wapiga kura na siyo viongozi wa kesho..,

ni aina ya siasa ambayo imejaa watawala na siyo viongozi.., udikteta kwa hao watawala ni mkubwa na ukandamizaji kwa wale walio Chini ya watawala hao ni mkubwa..., labda sasa, BEN ameamua kujiweka mbali ma siasa kwa muda huu ili atimize malengo yake ya kupata shahada yake ya 3 (PhD).., ambayo yuko mbioni kuweza kuikamata..,

Lakini.., BEN hajaanza leo harakati za kisiasa, amesoma wakati wote akiwa katika harakati hizo.., ametumikia elimu yake kwa weledi mkubwa sana na wakati huo akitumikia na siasa kwa wakati mmoja.., sioni namna hoja hii ikipata nguvu, kwa sababu, ndugu, jamaa na rafiki zake wangelikuwa wanajua alipo hadi sasa (kama suala ni kuachana na siasa kwa sasa)..,

USHAURI WANGU ;

(i) CHADEMA, kama waajiri wa zamani wa Ben Rabiu wa Saanane, wanapaswa kutumia idara yao ya sheria kutafuta haki mahakamani ya kuomba kibali cha maiti zile ambazo ziliokotwa mto Ruvu na kuzikwa Bagamoyo (zifanyiwe uchunguzi wa kitabibu) kubaini sampuli za wale marehemu kwa kufananisha hata na ndugu zake na BEN.., (itasaidia kuachana na wazo hilo)

(ii) ifunguliwe kesi mahakamani, kupitia ndugu zake na BEN (Familia) na msaada wa taasisi ya kisiasa ambayo BEN amehudumu kama mtumishi wake, kuwalazamisha polisi na TCRA (mamlaka ya mawasiliano nchini) kufanya uchunguzi yakinifu wa wapi BEN ametumia simu yake kwa mara ya mwisho, amewasiliana na nani na watu gani amekuwa akiwasiliana mao mara kwa mara, (taarifa hizo zipo katika server ya mtandao wa simu aliokuwa anatumia BEN)

(iii) wanachama wenzake na BEN, marafiki zake.., wanapaswa kuanzisha vuguvugu hai la kumdai mwenzao (mwanachama mwenzao) kwa uongozi wa chama chao (hata kama haujui alipo) ili chama kitoe msaada anuwai wa kusema kwa sauti na kuchukua hatua anuwai za kudai na kushinikiza umma utambue upotevu wa mwenzao na hivyo vyombo vya dola, ulinzi ma usalama vitumie wakati na muda wao kwa nguvu sana kumtafuta mtanzania huyu..

(iv) bila kuchoka, wananchi, ndugu, jamaa na marafiki wa BEN na wale wote ambao wanaguswa na tukio hili, waendelee na kampeni kubwa mitandaoni kwa kutumia hashtag maalum za kuonesha kumhitaji BEN.., zipo nyingi, mfano  #BRINGBACKOURBEN  #WENEEDOURBENBACK #BRINGBACKBRNALIVE #TUNAMTAKABENWETU na nyingine nyingi..  Hizi hashtag zinafikisha ujumbe kwenye jamii ya Dunia kwa haraka sana..,

(v) vyombo vya ulinzi na usalama (kupitia jeshi la polisi), lina- wajibu mkubwa sana wa kulinda usalama wa raia na mali zao, hivyo, wanapaswa kutoka hadharani, (hii habari ya kupotea kwa mtanzania kwa siku 32) ndani ya nchi yake, siyo habari ndogo, ni habari kubwa kweli-kweli.., inaweza kuchafua taswira ya taifa letu.., hivyo jeshi la polisi litoke nje hadharani na kueleza umma kuhusu mwenendo wa tukio hili (kuondoa hofu tanduzi katika vichwa vya marafiki, ndugu, jamaa wa Ben) Ben ni raia, hivyo jeshi la polisi lina wajibu wa kuwajibika kwa mtanzania huyu (mlipa kodi halali wa taifa hili)

MWISHO: i. Chama cha Demokrasia na maendeleo ambapo Ben amekuwa mwanachama na kiongozi, hatua ya kutoa tamko mara moja na kisha kukaa kimya haitoshi ikilinganishwa na umuhimu na na juhudi za Ben katika kukijenga chama hicho kama mwanachama na kiongozi / mfanyakazi katika makao makuu ya chama.

ii. Swala lililokaa kisiasa kama hili serikali kutokuchukua hatua kubwa zinazoonekana katika macho ya wananchi linatia mashaka hasa kwa wanaharakati ambao kupitia ukosoaji wao serikali inapata kujua maeneo ambayo inahitaji kufanyia marekebisho katika utendaji kiurahisi.