Saturday, 27 October 2018

Birthday Party (Isaya J Ngeleja)

Na Mwandishi wetu: Nascent Franzwa
Sat 27 Oct 2018 maeneo ya Artisan Kagera Sugar katika mkoa wa Kagera majira ya usiku unategemewa kuwa usiku Wa aina yake.

Hii ni kutokana na tukio la aina yake kuwahi kufanyika kama kumbukumbu ya birthday kutegemewa kufanyikia hapo.

Isaya Ngeleja (Graduate Trainee) kiwandani hapo anategemewa kufanya kumb. ya kuzaliwa kwa namna ambayo imeelezwa kuwa kufuru eneo hilo.
Usikose kufuatilia tukio hilo litakarushwa mubashara na Marambamedia

Saturday, 22 September 2018

AJALI MV NYERERE MAJONZI MWANZA

20 September 2018 majira ya Saa nane alasiri iligeuka simanzi jijini Mwanza na viunga vyake.
Hii ni baada ya kivuko cha MV Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Buhorora Ukerewe na Ukara (visiwani) kupata ajali kikiwa kinakaribia kabisa kutia nanga.Imeelezwa kuwa kivuko hicho huenda kilibeba uzito zaidi ya uwezo wake kwani hata idadi ya maiti zilizookolewa ni zaidi ya 131 huku walio hai wakiokolewa takribani 40 + Injinia mmoja aliyeokolewa baada ya siku mbili (Sept 22)
Kinachoshangaza ni kuwa vyombo vya usafiri majini huwa na mstari mweusi au mwekundu ambao haupaswi kuzama wote majini.Mstari kama ungeangaliwa kabla ya safari kuanza huenda ungesaidia kuona kama uzito umezidi au la hasha.Bado haijabainika kama ukaguzi huo ulifanyika.
Ni vema pia katika karne hii ya sayansi na technolojia kukawekwa madaraja ya kupimia uzito/Weight bridge/Mizani katika bandari zetu kama Bado hatujafanya hivyo ili kupunguza uwezekano wa ajali za uzembe kutokea kutokana na ukadiriaji wa kizamani.
Mungu azilaze roho za marehemu wetu mahali pema peponi.Amina

Sunday, 6 May 2018

Tanzia

May 6, 2018 ni siku moja kabla ya kuanza kwa mitihani ya kidato cha 6 nchini Tanzania, mwanafunzi mmoja ajiua kwa kujinyonga katika mti wa mwembe.

Mwanafunzi huyo Robert Masaba (21) ni mmoja wa wanafunzi waliohamishwa kutoka shule ya sekondari Nyakato manispaa ya Bukoba kwenda Kahororo baada ya shule ya Nyakato kuharibiwa na tetemeko lililokumba mkoa wa Kagera miaka 2 iliyopita, lililoanza mnamo 10 September 2016.

Aidha,mwanafunzi Robert(marehemu) mwenyeji wa wilaya ya Kwimba mkoa wa Mwanza alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliotegemewa kuanza mitihani yao ya kuhitimu kidato cha sita hapo kesho 2018 May 7.

Bado haijathibitika kwanini ameamua kufanya kitendo hicho kilicho kinyume na haki ya kuishi.
Mungu awasaidie waliobakia wafanye vema mitihani yao.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa; jina la Bwana na libarikiwe.

The Death of Death "Mwisho wa Kifo"

Kifo kitakuwa uamuzi kufikia mwaka 2045!!!!
Kufariki itakuwa 'chaguo' ndani tu ya miaka 27 na  mlolongo wa kuzeeka utakuwa 'unaogeuzika', kwa mujibu wa WAHANDISI JENITIKI WAWILI wakati wa uwasilisho wa kitabu chao kipya Barcelona.

José Luis Cordeiro, alizaliwa Venezuela na wazazi Wahispania, na Cambridge (UK) mwanamahesabu David Wood, mwanzilishi wa operating system 'Symbian', wamechapisha "The Death of Death" ie KIFO CHA KIFO au mwisho wa kifo kwa tafsiri isiyo rasmi, na kusema kutokufa ni sahihi na uwezekano wa kisayansi ambao ungekuja mapema zaidi zaidi ya ilivyofikiriwa awali.

Binadamu watafariki tu kwa ajali, kamwe si kwa asili ama ugonjwa, kufikia mwaka 2045, walisema Cordeiro na Wood, ambapo walisema ni 'muhimu' kwamba uzee unaanza kuainishwa kama  'ugonjwa' ili kwamba ufadhili wa umma katika tafiti juu ya 'tiba' yake uongezwe.

Nanoteknolojia ni ufunguo, kati ya mbinu nyingine mpya za uendeshaji vinasaba, Wahandisi walisema wakati wa uwasilisho wakiwa "Equestrian Circle "Barcelona.

Mchakato utahusisha ugeuzaji jeni 'mbaya' kuwa jeni bora, kuondoa seli zilizokufa mwilini, kukarabati seli zilizoharibiwa, matibabu kutumia seli za shina na 'kuchapisha' ogani muhimu katika 3D.

Cordeiro, ambaye yupo Massachusetts Institute of Technology (MIT) USA, alisema amechagua " Kutokufa" na kwamba katika kipindi cha miaka 30, atakuwa 'mdogo zaidi ya alivyo hivi sasa'.

Kuzeeka ni matokeo ya mikia ya DNA , iitwayo 'telomeres', katika kromosomu –ambapo kila seli isipokuwa seli nyekundu za damu seli jinsia, zina jozi 23 – zikifupika, na kukengeusha uzee  kunahusisha urefushaji wa telomeres.

Telomeres huharibika na kufupika kadiri muda usongavyo, mchakato uongezao kasi ya tukio la sumu kuingia mwilini– uvutaji, vileo na uchafuzi hewa ni kati ya mambo yanayoathiri urefu wa telomeres, hivyo kuchochea kuzeeka.

Cordeiro na Wood wanaamini kuwa  ndani ya miaka 10 , magonjwa kama  kansa yatakuwa yakitibika, na kwamba mashirika makubwa ya Kimataifa kama Google yataingia katika uwanja wa kitabibu "medicine" kwa sababu yanaanza kutambua kuwa "kutibu  kuzeeka inawezekana".

Microsoft tayari wameripoti kutengeneza kituo cha cryopreservation ambapo  Wanasayansi wanatafiti uwezekano wa kansa kutibika kabisa ndani ya muongo mmoja.

Wahandisi walielezea kuwa, ingawa 'watu kiujumla hawaelewei juu ya hilo', iligundulika mwaka 1951 ni namna gani seli kansa ni salama: wakati Henrietta Lacks alipofariki kwa kansa ya shingo ya kizazi "cervical cancer", upasuaji ulipoondoa tumor na kuihifadhi– na bado ipo  'hai' hivi sasa.

Kutokufa hakutamaanisha  sayari itazidiwa idadi ya watu, wanasayansi walisema: Bado kuna nafasi watu wengi duniani, na siku hizi, hakuna popote watu wenye watoto wengi kama ilivuokuwa kwa miongo na karne  zilizopita ; pia, 'itawezekana kuishi anga za mbali wakati huo'.

“Japan na Korea, kama wataendelea na tabia yao ya sasa ya kutokuzaa, watapotea kabisa – ndani ya karne 2, hakutakuwa na Mjapani au Mkorea duniani,” Alisema Cordeiro.

“Lakini asante kwa hii mbinu mpya, kweli wataendelea kuwepo Wajapani na Wakorea, kwa sababu wataishi milele na kubakia vijana.”

Gharama ya matibabu ya kuzuia uzee inalinganishwa na  ile ya  SimuJanja za karibuni.

“Mwanzoni, itakuwa ghali, lakini kwa soko shindani bei itapungua taratibu kwa sababu kitu kimnufaishacho kila mmoja,” Alisema Cordeiro.

“Teknolojia, ikiwa bado mpya, ni dhaifu na gharama sana, lakini hatimaye huwa ya kidemokrasia na kutawala na kuwa rahisi.”

Wahandisi wamesema kuwa tayari wamewekeza mbinu zao miaka 2 – kiharamu, lakini Colombia ambapo kuna taratibu chache zinazohusu uendeshaji genitiki.

Elisabeth Parrish, mgonjwa wao wa kwanza, 'alianza kuona dalili za kuzeeka na kuuliza kipi kingaliweza kufanyika ili kuzuuzuia'.

Matibabu yake ni 'hatari sana na haramu pia', Wood alieleza, lakini hivi sasa anaendelea vema, hayajatokea madhara yoyote yatokanayo na matibabu, na kiwango cha telomeres katika damu yake ni 'miaka 20 kiudogo zaidi ya kabla ya matibabu'.

“Nataka Hisapania iwe na  sehemu katika dunia ya hii mbinu na kuonesha kuwa sisi sio vichaa, ni vile watu bado hawawafahamu,” Wood alihitimisha.

Mwisho wa kifo "The Death of death" hatimaye kitachapishwa katika lugha nne kwa mara ta kwanza– Kihispania/Kihispaniola, Kingereza, Kireno na Kikorea – na mspato yote toka kwa mauzo yake yatawekezwa kwa  utafiti wa mwandishi.

 IMETAFSIRIWA NA Nascent Franzwa
nascentfrancium@yahoo.com
B.Sc Agriculture General
" Self-Proclaiming Extension Officer "

Saturday, 11 November 2017

Mh Rais Magufuli azuru KSL

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Joseph Pombe Magufuli alikuwa Rais wa kwanza kuzuru kiwanda cha kuzalisha sukari, ambapo Kagera Sugar imepata bahati hiyo katika kipindi cha takribani miaka 14 pasipo viwanda vya sukari kupata bahati hiyo.
Siku ya Jumatano tarehe 8 November 2017, siku mbili baada ya uzinduzi wa jengo la kisasa la abiria la uwanja wa ndege wa Bukoba.
Rais Magufuli ambaye amejipambanua kwa Sera ya Viwanda, amekuwa akihubiri Maendeleo ya uchumi wa kati ambayo amejizatiti kuyafikia kupitia uimarishaji wa Sera ya Viwanda ili Tanzania iweze kuneemeka moja kwa moja na rasilimali nyingi ilizo nazo.
Aidha, pamoja na kukimwagia kiwanda cha Kagera Sugar sifa nyingi, pia aliwaomba wamiliki wa viwanda vya sukari nchini Tanzania kumhakikishia kutokuwepo kwa upungufu wa sukari nchini,ambapo pia aliwapa nafasi ya kuchukua tenda ya uagizaji wa Sukari msimu usiokuwa wa uzalishaji Sukari nchini.Kwa kuwapatia vibali hivyo, Rais ana imani kuwa  ataweza kuzuia mianya ya uagizaji holela wa Sukari nje ya nchi ambayo inapelekea baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu kuagiza Sukari isiyokuwa na ubora.

Aidha pia, Rais aliwaomba wazalishaji wote wa Sukari kuona ni namna gani wataweza kuongeza uzalishaji wa Sukari ili watakapofikia kiwango cha mahitaji kwa Taifa, aweze kuzuia kabisa uagizaji wa Sukari toka nje ya nchi.
Kiwango cha mahitaji ya sukari  kwa Mwaka ni takribani tani 450000 na upungufu takribani tani 130000.

Baada ya ziara hiyo Rais aliendelea na ziara yake ambapo alizuru taifa jirani la Uganda.

Friday, 3 March 2017

AJALI YA BASI YALETA MAJONZI SUA

Usiku wa Alhamisi ya tarehe 2 Feb 2017 uligeuka simanzi kwa Watanzania baada ya basi la abiri mali ya kampuni ya Ilyana kutokea Dar kwenda Songea kupata ajali maeneo ya Njombe .

Katika ajali hiyo watu watatu walipoteza maisha huku 28 wakijeruhiwa.Aidha, kati ya waliopoteza maisha, mmoja ni mwanamke na wawili ni wanaume.

Chanzo chetu cha habari kimeweza kupata jina la mmoja wa wanaume waliopoteza maisha kuwa ni Festo Nungu, ambaye alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa mwisho katika Chuo kikuu cha Sokoine, katika Koleji ya Agriculture akiwa amebakisha semester moja kuhitimu shahada ya Kilimo mseto.

Mwenyezi Mungu azipumzishe roho za marehemu wote pema peponi.
Bwana alitwaa Bwana ametwaa, jina la Bwana libarikiwe.Amina

Sunday, 12 February 2017

BARUA YA WAZI KWA RAIS

BARUAKWENDA KWA RAIS JPM ILIYOANDIKWA NA ANSBERT NGURUMO

Mheshimiwa Rais John Magufuli, sijawahi kukuandikia barua, ama ya sanduku la posta au ya mtandaoni. Leo nakuandikia kupitia gazetini kwa sababu mbili:-

Kwanza, natambua kuwa wewe ni msomaji wa magazeti. Naulishanithibitishia kuwa hukosi kusoma maandishi yangu. Kwa hiyo najua utasoma.

Bahati nzuri, ninachokuandika si siri. Ni barua ya wazi itakayosomwa na Watanzania wengine. Lengo la kuiweka wazi ni kukuhamasisha nawe utambue kuwa mawasiliano ya kujenga nchi hayahitaji kufanyikia sirini au gizani.

Hii itakufanya uelewe kwanini wananchi hawachoki kuhoji sababu za serikali yako kufuta matangazo ya bunge ya moja kwa moja. Nakwambia bila kificho kuwa, hata mjieleze vipi, wananchi hawako tayari kuelewa kuwa katika karne hii, bunge lao linaondolewa kwenye nuru na kuingizwa kwenye giza.

Mwanzoni, wananchi, wakiongozwa na wabunge, walimkasirikia Nape Nnauye, waziri uliyempa dhamana ya habari, sanaa, utamaduni na michezo, wakidhani ndiye aliamuru TBC, Shirika la Utangazaji la Taifa, lisitishe matangazo ya moja kwa moja kwa kisingizio cha gharama; kwa sababu ndiye aliyetoa tangazo hilo bungeni.

Lakini sasa wanaelewa kuwa Nape hawezi kufanya uamuzi mkubwa kama huo bila kutumwa na mkubwa wake wa kazi. Na kwa jinsi wanavyokufahamu wewe, kama Nape angekuwa amefanya uamuzi huo wa kijinga bila kukuhusisha au bila kutumwa na wewe, ungekuwa ama umetengua uamuzi huo au umemtumbua jipu.

Kwa sababu hiyo, wananchi wameachanana Nape, wanakuandama wewe, na sasa wanasema jipu hilo ni lako. Unaogopa kujitumbua kwa kuwa mganga hajigangi. Ndiyo maana nimeamua nikutumbue.

Pili, mimi na Watanzania wamegundua kuwa katika masuala mengi ya kitaifa, unadanganywa. Vijana wa mjini wanasema unaingizwa mkenge. Na ukishadanganywa, nawe unaibuka na kudanganya wananchi.

Naomba utambue kuwa kwa kusema haya siombi kazi kwako. Ninayo. Na sehemu ya majukumu yangu kwa taifa hili ni kuuambia wewe ukweli mchungu bila woga au upendeleo.

Tabia yangu hii inasaidia kuziba mapengo ya wasaidizi wako ambao, licha ya kwamba wapo katika majengo wanayoita ofisi, kimsingi hawapo kazini, kwa kuwa hawafanyi kazi yao, hasa ya kukushauri viizuri.

Na baadhi yao wanasema kwamba hushauriki, unafanya utakalo, mara nyingi, bila kupima madhara ya uamuzi wako.

Wanasema hii ndiyo sababu inayokufanya utoe kauli tata au zinazopingana mara kadhaa.

Kwa mfano, mtu mmoja ameandika kwenye mtandao wa kijamii, akinukuu kauli yako uliyotoa kwa hasira mwezi Februari 2016 baada ya MCC, Shirika la Changamoto za Milenia, la Marekani, kukata misaada kwa Tanzania kwa sababu ya wizi wa kura Zanzibar na kutunga sheria katili ya makosa ya mtandaoni.

Siku ile, ulisema hivi: “Haiwezekani nchi tajiri kama Tanzania tuwe ombaomba. Sisi ndio tunatakwa kuombwa misaada.”

Kauli yako ilizua gumzo nchi nzima. Baadhi ya wananchi, wakiwemo marais wastaafu, walisema kuwa misaada kutoka nje haikwepeki, na kwamba hata kama kauli yako ina ukweli wa kimantiki, si kweli katika uhalisia kwa kuwa serikali yako, haijajipanga kujitegemea na kujitosheleza.

Wengine walikudhihaki kuwa umetoa kauli hiyo mithili ya simulizi la sungura aliyeruka akashindwa kufikia mkungu wa ndizi, hatimaye akasema kwa hasira, “sizitaki mbichi hizi!!”

Vibaraka wako, wakiwamo wasaidizi wako, walitetea hoja yako. Mungu si Athuman, juzi umetoa kauli nyingine ulipotembelewa na Balozi wa Mareakani nchini, akaahidi kuipatia serikali yako msaada mkubwa wa dola milioni 800.

Katika furaha uliyokuwa nayo, ulisema hivi mbele ya waandishi wa habari:

“Amekuja balozi kutuhakikishia kwamba watatoa hela kwa ajili ya Tanzania, na anasema sasa hivi watatoa zaidi ya dola milioni 800, na mkataba mwingine tunaweza kusaini hata kesho wa dola milioni 410….Fedha za msaada kutoka Marekani ni muhimu mno kwa maendeleo ya Tanzania.”

Tuna marais wangapi? Februari ulisema hutaki misaada; Juni unasema misaada ni muhimu. Tunapouliza wasaidizi wako kwanini wanakuacha unatoa kauli za ajabu ajabu, wanasema hupendi kushauriwa.

Wanasema kuwa wanaogopa kukuambia usichotaka kusikia, kwa sababu wameshakusoma, unapenda kusikiliza sauti yako mwenyewe na kutanguliza hisia zako, badala ya kufanyia kazi ushauri wa wataalamu.

Eti wakati mwingine wanakuandikia hotuba za kirais katika matukio muhimu, ukishafika eneo la tukio unagoma kuzisoma; unatoa maoni yako ya kichwani, ambayo wakati mwingine yanakufanya uonekane kama kamanda wa polisi bada ya rais wa nchi.

Wanasema, kwa mfano, siku ya maadhimisho wa Wiki ya Sheria, maneno uliyotoa mbele ya wanasheria waliobobea, huku ukimwagiza jaji mkuu, yalikuwa yamekataa tenge, na hayatekelezeki kisheria; ni amri zisizofanana na mfumo wa kidemokrasia na utendaji wa kisheria.

Hawakukuambia pale pale, lakini walikuteta baadaye. Kwanini unaruhusu mambo haya yatokee wakati una nyenzo za kuyazuia?

Mmoja ameniambia wiki hii kuwa kwa jinsi anavyoona unazungumza na unatenda, una nia nzuri na taifa hili, lakini unakosa mbinu za kiuongozi. Anasema unatenda kama meneja, si kiongozi.

Anasema vitu vingine unavyoagiza, au unavyoamua, unavifanya kama mtawala, si kama kiongozi. Na kwa kukosa tunu ya uongozi, utafanya mambo mengi mazuri juu juu lakini hayatadumu kwa sababu hayakujengwa juu ya msingi imara.

Utakuwa umefanikiwa kufanya mambo mema kwa muda mfupi, lakini yatafutika kirahisi kwa kuwa mtindo uliotumika kuyatekeleza si endelevu, bali zima moto.

Wasaidizi wako wanakuficha mambo ya msingi. Wanasema umezidi ukali, na huna subira wala simile, kiasi kwamba unaweza kumwaibisha mtu yeyote mahali popote, bila kujali cheo au hadhi yake.

Na unawafanyia wenzako hivyo, lakini wewe hutaki kuguswa au kusahihishwa. Unalinda cheo chako, unadhalilisha vyeo vyao.

Kama ulikuwa hujajua, washauri wako sasa wana msimamo rasmi, kwamba watakushauri kwa kuzingatia kile unachotaka kusikia kutoka kwao.

Kama msimamo huu utadumu, mheshimiwa rais utaangamiza nchi. Kama unafurahia kuongoza nchi ya watu waoga, ujue nchi hiyo si Tanzania tunayotaka kujenga, au ile unayozungumzia kwenye hotuba zako.

Mazuri yote unayohubiri kwenye hotuba zako, yatatumika kukukejeli baada ya muda wako wa kukaa Ikulu kuisha.

Wanakutii, lakini hawakupendi. Na kwa sababu unawapuuza, wakipata fursa watakuhujumu.

Hata hivyo, wapo pia wanaodhani kwamba huna washauri wazuri. Mtu mmoja amesema; “Tatizo ninaloona sasa hivi, wasaidizi wa rais wanashindwa kutafsiri dira na ajenda yake. Hawamwelewi, naye haeleweki kwao.

“Apende asipende, anahitaji semina elekezi. Uamuzi unaochukuliwa na wasaidizi wake unatokana na tafsiri yao ya dira yake. Wengi wanafanya kwa woga na kulinda ajira zao tu.

“Panapohitajika ushauri wa kitaalamu wanapatwa na ugonjwa wa kupooza, kwa sababu wanaangalia matokeo ya kisiasa na uhusiano wao na rais. Tuanze kujiuliza, rais anaposema ‘Hapa Kazi Tu, ana maana gani?”

Huyu alisema hivi baada ya jeshi la polisi kuzuia mikutano ya wanasiasa kwa sababu zile zile za miaka nenda rudi. Hawakui. Hawaelimiki. Na baadhi ya wakuu katika jeshi la polisi wanadai kuwa “wamefanya hivyo kwa kufuata “maagizo kutoka juu.” Huko juu ni wapi kama si Ikulu?

Uamuzi huu wa kuzuia mikutano ya vyama vya siasa, kwa hofu kwamba itawafanya wananchi waelewe udhaifu wa serikali ya awamu ya tano, na kukuza upinzani ambao umesema mara kadhaa kwamba una nia ya kuuua, unakutia doa.

Uamuzi huu unakuondolea taswira ya ujasiri unayojijengea majukwaani unapokuwa unafoka. Sasa wananchi wanahoji: “Kumbe anafoka kuficha udhaifu wake!”

Ushauri, wangu kwako ni huu: Ongoza nchi, usiitawale. Acha wananchi wapumue. Zungumza nao, usiwahutubie. Sikiliza washauri wasiojikomba kwako.

Kumbuka kuwa nchi hii si ya rais na baraza la mawaziri, bali ni ya wananchi uliokuwa unawaomba kura na kuwaburudisha kwa maneno matamu na pushapu jukwaani. Hawa ndio waajiri wako. Wasikilize. Jifunze kwamba ubabe hautawali nchi yotote katika karne ya sasa.

Wananchi wanatazama mbele, hawatakubali kurudishwa nyuma, hata kwa mabavu