Trump aidhinishwa rasmi kuwa Rais wa 45 wa Marekani.
Siku 32 za kupotea kwa Mwanaharakati wa Chama Kikuu cha upinzani nchini Tanzania , CHADEMA ,Ndg Ben Saanane bado ni fumbo zito.
Balozi wa Urusi nchini Uturuki Bwana Andrey Karlov auawa kwa kupigwa risasi akiwa katika ufunguzi wa maonesho ya sanaa. Rais Vladimir Putin amekitaja kitendo hicho kama uchokozi.
Mkurugenzi mtendaji wa mtandao maarufu Afrika Mashariki na Kati Jamii Forum Ndugu Maxence Melo aachiwa huru kwa dhamana huko nchini Tanzania.
Nchini DRC milio ya risasi imesikika maeneo kadhaa ya miji ikiwemo miji nikiwa ya Kinshasa na Lubumbashi kutokana na kutokuelewana kati ya upinzani na serikali juu ya muda wa nyongeza wa Joseph Kabila kusalia madarakani baada ya muhula wake kuisha usiku wa kuamkia Leo 20 Dec 2016.
Ripoti za shirika la Afya duniani zimeeleza kuwa, idadi inayokadiriwa kuwa sawa na nusu ya watu wazima barani Afrika wanakabiliwa na tatizo la Shinikizo la damu (Pressure) na hivyo kuifanya Afrika kuwa na kiwango cha juu cha tatizo hilo duniani kwa mujibu wa WHO.
Katika Michezo: Mwanadada Evelyene Njambi Thungu kutoka Kenya ameingia katika orodha ya warembo watano bora katika shindano la Malkia wa urembo duniani 2016 lililofanyika huko Marekani. Kwa sasa ndiye Malkia wa urembo barani Afrika.
No comments:
Post a Comment