Feb 10 2017 nilipata bahati ya kutembelea hifadhi ya Taifa ya wanyama nchini Tanzania ijulikanayo kama Mikumi.
Mikumi ni hifadhi ya 4 kwa ukubwa ikitanguliwa na Serengeti, Ngorongoro na Manyara.
Hifadhi hii ipo katika mkoa wa Morogoro kati ya barabara iendayo Iringa.Ni hifadhi iliyosheheni wanyama wengi wa porini ikiwemo jamii ya swala,nyati,nyumbu, pundamilia, tembo, twiga, Simba na Chui.
Kilichonivutia zaidi ni juu ya Twiga.Huyu ni mnyama mwenye uwezo mkubwa wa kutofautisha rangi mbalimbali ikilinganishwa na wanyama wengine.Wao huweza tu kutofautisha nyeupe na nyeusi.
Mnyama huyo anapoona kitu kigeni hutulia mithili ya sanamu kwa ajili ya kuweza kukitambua na kama ni adui aweze kujua namna ya kujihami.
Kinachovutia zaidi ni mwondoko wake hasa anapotembea mwendo wa pole. Kutokana na muundo wa shingo yake pamoja na miguu yake, atembeapo mnyumbuliko Wa mwili wake huvutia mithili ya mwanadada mrembo awapo katika kupita mbele ya majaji ili apate kura za unenguaji.
Pamoja na hayo yote, Moyo Wa twiga huweza kukua hadi kufikia kilo 12 na hivyo hii humfanya kushindwa kuwa na mzunguko mzuri wa damu endapo atalala. Ili kuepusha shida, alalapo hukunja miguu na kulalia kifua, huku shingo ikiwa juu ama kuegeshwa kwenye mti.
No comments:
Post a Comment