Tuesday, 12 July 2016

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA BAADA YA CR7 NA TIMU YAKE KUREJEA URENO


 3627C74B00000578-3684274-The_Portugal_bus_arrives_at_the_airport_as_the_country_s_heroes_-a-114_1468241690596

Usiku wa 2016 July 10 timu ya taifa ya Ureno ilifanikiwa kushinda Kombe la mataifa ya Ulaya a.k.a Euro, kwa kuinyuka timu ya taifa ya Ufaransa goli 1-0, goli ambalo lilifungwa na na Eder dakika ya 109 katika uwanja wa Stade de France.
3627C23900000578-3684274-Ronaldo_and_Nani_enjoy_the_celebrations-a-119_1468241690836
Baada ya ushindi huo July 11 2016 kikosi cha timu ya taifa ya Ureno kiliwasili Lisbon Ureno wakiwa na Kombe lao na kupata mapokezi makubwa kutoka kwa raia wa nchi hiyo, Ronaldo na wachezaji wenzaji waliwasili Ureno na kutembeza Kombe wakiwa katika basi la wazi.
Tazama picha hapa chini kisha tuambie kipi kifanyike kwa timu ya Taifa TANZANIA yaani TAIFA STARS ili siku moja macho yote Africa yaelekezwe Tanzania


3629C5E100000578-3684274-image-a-143_1468244718738


3628CB1900000578-3684274-Cristiano_Ronaldo_holds_aloft_the_European_Championship_title_af-a-116_1468241690686

Pamoja na kuwa Ufaransa waliweza kusakata kabumbu safi mwisho wa dak 120 ushindi ulilazimika kwenda kwa mshindi kwani ndivyo zilivyo sheria za soka duniani.





UHARIBIFU DARAJA-KIGAMBONI


JE, UMEIKOSA VIDEO FUPI YA UHARIBIFU ULIOTOKEA BAADA YA LORI KUPINDUKA DARAJA LA KIGAMBONI?
 
Ilitokea ajali ya Lori lililokua na Kontena kwenye daraja la Nyerere Kigamboni Dar es salaam usiku wa kuamkia July 11 2016 ambapo ajali hiyo imesababisha majeruhi pamoja na eneo la barabara kuharibiwa, Meneja msimamizi kwenye hili daraja Gerald Sondo alipohojiwa kuhusiana na ajali hiyo alisema tangu daraja hilo maarufu kama Daraja la Nyerere kuanza kutumika hiyo ilikuwa ajali ya kwanza kubwa kuwahi kutokea katika daraja hilo. Ajali hiyo ilisababishwa na gari aina ya SEMI TRAIOLER iliyoacha njia yake na kuzigonga kingo za barabara mojawapo katika flyover (Mandela Road)
Gari hilo lilikuwa likitokea  maeneo ya kigamboni kuelekea mjini. Kutokana na kanuni na taratibu za usimamizi wa daraja hilo, Meneja msimamizi alisema kuwa Uongozi utafanya tathmini ya uharibifu ili matengenezo yaweze kufanyika, lakini pia akasisitiza kuwa baada ya taratibu za kiserikali na kipolisi kukamilika, mhusika aliyesababisha ajali hiyo atawajibika kulipia gharama zote za matengenezo.,,,,,...Tembelea link hapa nchini kwa maelezo zaidi
http://youtu.be/-Wa2GqzcIC4

Monday, 11 July 2016

Ex-St Joseph njaa

WAHANGA WA MKASA WA ST JOSEPH WAMALIZA SEMESTER BILA ''......
Mnamo tarehe 19 Feb 2016 tume ya vyuo vikuu ilifungia vyuo shiriki viwili vya Chuo kikuu cha Mt Joseph kutokana na kushindwa kutekeleza matakwa ya mkataba wa utoaji elimu hapa nchini Tanzania.
Kutokana na hatua hiyo ya serikali kuvifungia vyuo hivyo vishiriki ambavyo ni St Joseph University College of Agricultural science and Technology, Songea na St Joseph University College of Information Tehnology, Songea, ililazimika wanafunzi hao kuhamishiwa katika vyuo vikuu vingine ambavyo ni SUA, RUCU pamoja na UDOM.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida,wakati vyuo vishiriki hivyo vikifungwa serikali kupitia TCU yaani Tanzania Commission of Universities iliahidi kuwa wanafunzi wangelipwa gharama zote za uhamisho jambo ambalo limegeuka kuwa kitendawili kisichojibika....Sambamba na hilo jambo linalotusikitisha sana uongozi wa Maramba media kama wadau wa elimu Tanzania ni kuwa tangu wanafunzi hao wahamishwe hadi wakati tukichapisha habari hii, zaidi ya wanafunzi 300 walio kati ya wanafunzi waliohamishiwa SUA hawajalipwa fedha zao za kujikimu kutoka HESLB ambayo ndiyo taasisi inayosimamia jambo hilo....Baadhi ya wanafunzi tuliohojiana nao wamedai kuwa hakuna majibu yoyote ya kuridhisha kutoka chuoni hapo wala HESLB......Kama wadau wa elimu Tanzania MARAMBA MEDIA tunapenda kutoa rai yetu kwa Waziri wa elimu Prof Joyce Ndalichako aweze kuliangalia jambo hili kwa mapana yake , pamoja na taasisi husika kwani pasipo hivyo Taifa litashindwa kufikia malengo.

Masanja Mkandamizaji mbioni kuitwa baba



MASANJA MBIONI KUITWA BABA MZAZI KWA WANAWE

    
 Hii imetokea kwenye ibada katika kanisa la miito ya Baraka Jangwani Dsm

Mchekeshaji,Muhubiri na Mshereheshaji Masanja Mkandamizaji push and shadow stelingi.shinyanga vijijini amvisha pete mke wake mbele ya macho ya Mwakibolwa.
Huu ni mfano bora kwa vijana wengi wa kileo ambao wamekuwa wakiaminishana kuwa kwa sasa hakuna haja ya kuoa.............Nini maoni yako?????????????

Sunday, 10 July 2016

BAVICHA KWENDA DODOMA

MBOWE AWATULIZA VIJANA WA BAVICHA

 

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mhe. Freeman Aikael Mbowe leo Jumapili 10/06/2016(jana) amewataka vijana wa CHADEMA nchi nzima waliokuwa wamejiandaa kuelekea mjini Dodoma kwa ajili ya kulisaidia jeshi la Polisi kuwaambia wanachama wa CCM kutii tamko lililotolewa na Rais Dkt. John Magufuli ya kufuta shughuli zote za siasa ikiwemo mikutano ya hadhara, mikutano ya ndani, makongamano n.k kutokwenda tena Dodoma mpaka utaratibu mpya utakapotolewa.
Akiongea katika semina ya Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri wanaotokana na CHADEMA jijini Arusha leo, Mbowe ametumia fursa hiyo kulitaka Jeshi la polisi kuacha kupendelea Chama kimoja, na waelewe kwamba Rais ni mwanasiasa, amechaguliwa kupitia Chama cha siasa, shughuli anazozifanya ni za kisiasa, Waziri Mkuu,Wakuu wa mikoa, wakuu wa Wilaya nao wanafanya shughuli za siasa.
"Nawataka vijana wote nchi nzima waliokuwa wanajiandaa kuelekea Dodoma, waache kwenda mpaka watakapojulishwa utaratibu mwingine kutoka ndani ya chama, kwa sababu Polisi wanapanga kufanya jambo ovu, kwani wameanza kuwakamata viongozi wa BAVICHA, waliokuwa wapo Dodoma, amekamatwa Patrobas Katambi ambaye ni Mwenyekiti wa BAVICHA na Julius Mwita ambae ni Katibu wa BAVICHA Taifa, wamekutwa wakila chakula wakakamatwa, kwa sababu Bwana Katambi ni Mwanasheria alitaka kujua kosa lake, lakini walimpiga, hili ni jeshi gani la Polisi lisilotambua wajibu, kulinda raia na mali zao" amesema Mhe. Mbowe.
Sheria ya vyama vya siasa na Marekebisho yake yote, yanatambua haki za vyama vya siasa kufanya shughuli zake za siasa bila kuvunja Sheria, huku Jeshi la Polisi likitoa ulinzi huo ukiwa ni wajibu wake.
Mbowe amesisitiza kwamba hawataomba tena kibali kwa jeshi la Polisi wala mamlaka yeyote, lakini wanabuni njia nyingine ya kufanya siasa, kwa sababu siasa ni maisha ya kila siku.
Wanakataza shughuli za kisiasa kwa sababu hawataki kukosolewa, wakati kuna mambo mengi sana ya kuikosoa Serikali, Serikali isiyotaka kukosolewa sio sikivu kwa wananchi inawaongoza.
Mhe. Mbowe amesisitiza kuwa wataendelea kupagania haki ya Taifa hili mpaka haki itakapotendeka, shauri lililokuwa limefunguliwa jijini Mwanza kupinga zuio la mikutano ya hadhara na maandamano jijini Mwanza, hivyo shauri hilo limehamkshiwa Mahakama Kuu Dar es salaam kupinga zuio la mikutano ya hadhara, maandamano, na shughuli mbalimbali, yakiwemo makongamano, mikutano ya ndani ya vyama vya siasa n.k.
Akiongea katika Semina ya Mameya na Wenyeviti wa halmashauri zinazotokana na CHADEMA, Mbowe amewataka wahakikishe wananchi waliowachagua wanawatumikia ipasavyo, kuhakikisha huduma muhimu zinapatikana kwa wananchi, kama afya,elimu n.k, Mbowe amewataka viongozi hao wawe wabunifu zaidi katika kutatua matatizo ya Wananchi waonyoshe tofauti kwa sababu Wananchi wamewaamini.
"Kuna tatizo kubwa sana la ajira nchini, hakikisheni mnatengeneza fursa za kutosha ambazo zitawapa vijana na watu wote ajira, maisha yamekuwa magumu maradufu, kila kukicha bora ya jana, nyie kama viongozi wa maeneo yenu kaeni na wananchi wenu, mbuni fursa ambazo zitawafanya wananchi wenu waweze kujikwamua kiuchumi" Amesema.
Pia Mhe. Mbowe amewataka Viongozi hao kuacha kutoa pesa kwa vyama vya siasa, watu wa CCM kuwekewa mafuta na kupewa pesa kutoka Halmashauri, kuanzia sasa, Mhe. Mbowe amewataka viongozi hao kuwanyima, na wakiendelea atawaumbua, Halmashauri hazitakiwi kutoa pesa kwa vyama vya siasa, iwe CCM,CHADEMA, CUF n.k.
Katika semina hiyo ambayo imefungwa Rasmi na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Mhe. Freeman Mbowe, pia umefanyika uchaguzi ambapo Meya wa jiji la Arusha,amechaguliwa kuwa Mwenyekiti,Katibu wake ni Meya wa Manispaa ya Kinondoni,na Mnadhim amekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tarime.
Viongozi hao watatu,wamekuwa Wajumbe wa Kamati Kuu.
Imetolewa Na: Kurugenzi Ya Habari Chadema



Ufaransa yaadhibiwa na Ureno

France Loses a Soccer Championship, but Achieves a Rare Unity

PARIS — Cristiano Ronaldo spends a lot of time alone. Alone on the wing, alone in his kitchen, alone in his thoughts, where, by his own admission, much of his focus is on whether he will again win the Ballon d’Or award — the world player-of-the-year honor, which, of course, is for a single, solitary superstar.
Ronaldo does not mind this (or, at least, he says he embraces it). Even by modern athletic standards, his entourage is necessarily small: his agent, his manager, a few close friends and his family. That is it. He often eats lunch by himself, often drives to practice by himself. Over the last 13 years, he has cultivated an image as someone who lives lavishly and luxuriously — estimates are that he is worth $320 million and so the pictures of him on a yacht are to be expected — yet also in relative quiet.
He has his 6-year-old son, Cristiano Jr. He has his agent and father or brother figure, Jorge Mendes. He has his soccer and his stardom and, depending on the particular parameters of the argument, his place on or near the top of the list of soccer’s greatest figures.
But here is the thing: Much of Ronaldo’s life is built upon his place at his club team, Real Madrid. This is not to say that Real Madrid is a house of loners or that there is no team spirit there; to the contrary, the club is strong and rich, and many of its supporters are passionate and devoted and true. But it is also undeniable that because of Madrid’s exorbitant resources — last year’s payroll was estimated at $180 million — there is a culture of stars, many of whom come and go. And Ronaldo, who has been the rare mainstay, is the brightest.
With Portugal’s national team, though, it is different. Ronaldo is still the biggest star, even more so than with Madrid, but the meaning of his presence, and the results, are not the same. On Sunday, Ronaldo will captain Portugal when it faces France in the final of the European Championships, the first time Portugal has been in a major final since it was stunned, on home soil, by Greece in the 2004 Euros.
Ronaldo was 19 then, a wunderkind who cried on the field after the final whistle. It was a brutal, bitter experience, but it did not stick to him, did not tarnish him. Neither did disappointing defeats in the semifinals of the 2006 World Cup or the 2012 Euros. In this era, results in international play are an additive to a player’s legacy, a bonus. Consider: Ronaldo and Lionel Messi are the near-universal choices as the best players in the game, yet neither has helped his country lift a significant trophy.
On Sunday at the Stade de France, that may change. Ronaldo has said, many times, that he craves a title for Portugal, that it is a dream for him. It is, presumably, a pure one, too: Winning will do little for Ronaldo financially. It will not make him more famous, either. Portugal has a population of a little more than 10 million; Ronaldo has six times that many Instagram followers.

Janga

PIGO KUBWA LATOKEA SUA

 
Picha ya Wardat Jampan
(marehemu)

Miezi michache baada ya mwanafunzi wa kiume wa mwaka pili chuo kikuu cha Sokoine katika kozi Sayansi ya chakula kupoteza maisha akiwa amelala maeneo ya mazimbu, pigo lingine limewapata tena wanafunzi wa chuoni hapo baada ya kumpoteza binti Wardat Jampan mwanafunzi wa ngazi ya cheti katika kozi ya IT......Binti Wardat aliyekuwa amelazwa katika hospitali ya Mazimbu inayomilikiwa na Chuo hi alifikwa na umauti jioni ya tarehe 10 July 2017, ikiwa ni masaa machache kabla ya siku ya kuanza mitihani ya mwisho wa mwaka kufika......Mwili wa marehemu ulisafirishwa usiku wa siku hiyohiyo kweda jijini Dar es Salaam kwa ajili ya maandalizi ya mazishi yatakayofanyika saa nne asubuhi kesho yake (Leo) tarehe 11/7/2016

Bwana alitwaa, Bwana ametwaa, jina la Bwana libarikiwe. Amina