MBOWE AWATULIZA VIJANA WA BAVICHA

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mhe. Freeman Aikael
Mbowe leo Jumapili 10/06/2016(jana) amewataka vijana wa CHADEMA nchi nzima
waliokuwa wamejiandaa kuelekea mjini Dodoma kwa ajili ya kulisaidia
jeshi la Polisi kuwaambia wanachama wa CCM kutii tamko lililotolewa na
Rais Dkt. John Magufuli ya kufuta shughuli zote za siasa ikiwemo
mikutano ya hadhara, mikutano ya ndani, makongamano n.k kutokwenda tena
Dodoma mpaka utaratibu mpya utakapotolewa.
Akiongea katika semina
ya Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri wanaotokana na CHADEMA jijini
Arusha leo, Mbowe ametumia fursa hiyo kulitaka Jeshi la polisi kuacha
kupendelea Chama kimoja, na waelewe kwamba Rais ni mwanasiasa,
amechaguliwa kupitia Chama cha siasa, shughuli anazozifanya ni za
kisiasa, Waziri Mkuu,Wakuu wa mikoa, wakuu wa Wilaya nao wanafanya
shughuli za siasa.
"Nawataka vijana wote nchi nzima waliokuwa
wanajiandaa kuelekea Dodoma, waache kwenda mpaka watakapojulishwa
utaratibu mwingine kutoka ndani ya chama, kwa sababu Polisi wanapanga
kufanya jambo ovu, kwani wameanza kuwakamata viongozi wa BAVICHA,
waliokuwa wapo Dodoma, amekamatwa Patrobas Katambi ambaye ni Mwenyekiti
wa BAVICHA na Julius Mwita ambae ni Katibu wa BAVICHA Taifa, wamekutwa
wakila chakula wakakamatwa, kwa sababu Bwana Katambi ni Mwanasheria
alitaka kujua kosa lake, lakini walimpiga, hili ni jeshi gani la Polisi
lisilotambua wajibu, kulinda raia na mali zao" amesema Mhe. Mbowe.
Sheria ya vyama vya siasa na Marekebisho yake yote, yanatambua haki za
vyama vya siasa kufanya shughuli zake za siasa bila kuvunja Sheria, huku
Jeshi la Polisi likitoa ulinzi huo ukiwa ni wajibu wake.
Mbowe
amesisitiza kwamba hawataomba tena kibali kwa jeshi la Polisi wala
mamlaka yeyote, lakini wanabuni njia nyingine ya kufanya siasa, kwa
sababu siasa ni maisha ya kila siku.
Wanakataza shughuli za
kisiasa kwa sababu hawataki kukosolewa, wakati kuna mambo mengi sana ya
kuikosoa Serikali, Serikali isiyotaka kukosolewa sio sikivu kwa wananchi
inawaongoza.
Mhe. Mbowe amesisitiza kuwa wataendelea kupagania
haki ya Taifa hili mpaka haki itakapotendeka, shauri lililokuwa
limefunguliwa jijini Mwanza kupinga zuio la mikutano ya hadhara na
maandamano jijini Mwanza, hivyo shauri hilo limehamkshiwa Mahakama Kuu
Dar es salaam kupinga zuio la mikutano ya hadhara, maandamano, na
shughuli mbalimbali, yakiwemo makongamano, mikutano ya ndani ya vyama
vya siasa n.k.
Akiongea katika Semina ya Mameya na Wenyeviti wa
halmashauri zinazotokana na CHADEMA, Mbowe amewataka wahakikishe
wananchi waliowachagua wanawatumikia ipasavyo, kuhakikisha huduma muhimu
zinapatikana kwa wananchi, kama afya,elimu n.k, Mbowe amewataka
viongozi hao wawe wabunifu zaidi katika kutatua matatizo ya Wananchi
waonyoshe tofauti kwa sababu Wananchi wamewaamini.
"Kuna tatizo
kubwa sana la ajira nchini, hakikisheni mnatengeneza fursa za kutosha
ambazo zitawapa vijana na watu wote ajira, maisha yamekuwa magumu
maradufu, kila kukicha bora ya jana, nyie kama viongozi wa maeneo yenu
kaeni na wananchi wenu, mbuni fursa ambazo zitawafanya wananchi wenu
waweze kujikwamua kiuchumi" Amesema.
Pia Mhe. Mbowe amewataka
Viongozi hao kuacha kutoa pesa kwa vyama vya siasa, watu wa CCM kuwekewa
mafuta na kupewa pesa kutoka Halmashauri, kuanzia sasa, Mhe. Mbowe
amewataka viongozi hao kuwanyima, na wakiendelea atawaumbua, Halmashauri
hazitakiwi kutoa pesa kwa vyama vya siasa, iwe CCM,CHADEMA, CUF n.k.
Katika semina hiyo ambayo imefungwa Rasmi na Mwenyekiti wa CHADEMA
Taifa Mhe. Freeman Mbowe, pia umefanyika uchaguzi ambapo Meya wa jiji la
Arusha,amechaguliwa kuwa Mwenyekiti,Katibu wake ni Meya wa Manispaa ya
Kinondoni,na Mnadhim amekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Tarime.
Viongozi hao watatu,wamekuwa Wajumbe wa Kamati Kuu.
Imetolewa Na: Kurugenzi Ya Habari Chadema