Usiku wa Alhamisi ya tarehe 2 Feb 2017 uligeuka simanzi kwa Watanzania baada ya basi la abiri mali ya kampuni ya Ilyana kutokea Dar kwenda Songea kupata ajali maeneo ya Njombe .
Katika ajali hiyo watu watatu walipoteza maisha huku 28 wakijeruhiwa.Aidha, kati ya waliopoteza maisha, mmoja ni mwanamke na wawili ni wanaume.
Chanzo chetu cha habari kimeweza kupata jina la mmoja wa wanaume waliopoteza maisha kuwa ni Festo Nungu, ambaye alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa mwisho katika Chuo kikuu cha Sokoine, katika Koleji ya Agriculture akiwa amebakisha semester moja kuhitimu shahada ya Kilimo mseto.
Mwenyezi Mungu azipumzishe roho za marehemu wote pema peponi.
Bwana alitwaa Bwana ametwaa, jina la Bwana libarikiwe.Amina